91. VIELEZI VINGINE VYA MAHALI
Hapa chini vipo vielezi vingine vya mahali:
ĉie= kila mahali, popote
nenie= popote (katika ukanushaji tu)
for = mbali fora = -a mbali (kivumishi)
Chungua matumizi ya vielezi hivi vya mahali katika sentensi zifuatazo:
Mi serĉos ĉie.
|
Nitatafuta kila mahali.
|
La homo vivas ĉie.
|
Yule mtu anaishi popote.
|
Mi trovis bananon nenie.
|
Sikukuta ndizi popote.
|
Mi venis el fora loko.
|
Nimetoka mahali pa mbali.
|
92. ZOEZI
Tafsiri:
Li ĉiam parolas bone. Mia kuzino neniam skribas
klare. Tiu virino ĉiam kantas gaje (gaj- = -enye
ukunjufu). Li parolas tre saĝe. Mi serĉis lin ĉie, sed trovis
lin nenie. Ili vivas tre simple. La ŝtelisto rapide kuris for. Mi ofte (mara
nyingi) vidis la ŝipojn. Li malofte uzas vortaron. Kompreneble, mi ne
iros.
93. MUUNDO WA MANENO
Sasa umeshaelewa kabisa muundo wa maneno tulioeleza pia
katika kifungu cha 5; bila shaka unafahamu kwamba kutoka mzizi VIV unaweza
kuunda maneno mengi, kwa mfano:
maisha
|
VIVo
|
(jina)
|
-enye uhai, -hai, -enye kuishi
|
-VIVa
|
(kivumishi)
|
kwa uhai, kwa maisha
|
VIVe
|
(kielezi)
|
kuishi
|
VIVi
|
(kitenzi)
|
niliishi, nimeishi
|
mi VIVis
|
(wakati uliopita)
|
ataishi
|
li VIVos
|
(wakati ujao)
|
atakayeishi
|
li, kiu VIVos
|
(wakati ujao)
|
n.k.
94. ZOEZI
Je, maneno mangapi unaweza kuunda kutoka mizizi ya hapa
chini?
am, esper,
telefon
Kwa mfano:
ami= kupenda, esperi = kutumaini, telefono
= simu,
sasa endelea wewe mwenyewe ukiandika maneno unayoyaunda
pamoja na tafsiri zao.
95. KIAMBISHI -U
Umeshajifunza msemo Diru al mi,"uniambie" (taz. kifungu cha
72). Basi, ukumbuke kwamba amri au matakwa au maombi unaweza
kutoa ukitumia kiambishi cha -u kwenye mzizi:
legu! soma! someni!
|
penu!
jaribu! jitahidi!
|
silentu! nyamaza!
|
skribu! andika!
|
lakini kwa upole na ukarimu itafaa kutumia msemo bonvolu...
-i, kwa mfano:
Venu al mi!
|
Njoo kwangu!
|
Bonvolu veni al mi!
|
Tafadhali njoo kwangu!
|
96. ZOEZI
Rudia sentensi zifuatazo ukitumia neno bonvolu:
Finu
vian taskon! (Maliza kazi yako! ), Atentu kaj aŭskultu! (Angalia
usikilize!), Ne rigardu al ŝi! (Usimtazame!), Ne parolu dum la
leciono! (Usizungumze wakati wa kipindi!).
97. VITENZI MAALUMU
ANGALIA sana ujifunze misemo ifuatayo:
Mi povas iri.
|
Ninaweza kwenda.
|
Mi devas iri.
|
Inanipasa kwenda. Au:
|
|
Inanibidi kwenda.
|
|
Yanilazimu kwenda.
|
|
Sina budi kwenda.
|
|
Ninalazimika kwenda.
|
|
Lazima niende.
|
|
Ni lazima niende.
|
Mi volas iri.
|
Nataka kwenda.
|
Mi deziras iri.
|
Napenda kwenda.
|
Mi ne povas iri.
|
Siwezi kwenda. (LAKINI: Siwezi = Mi ne bonfartas.)
|
Ĉu vi povos iri?
|
Je, utaweza kwenda?
|
Li ne povis iri, ĉu?
|
Hakuweza
kwenda, sivyo?
|
98. NENO JEN
UKIULIZA Kie la libro estas? au Kie estas la
libro? (Kile kitabu kipo wapi?) unaweza kujibu Jen ĝi estas! (Ndicho hiki! Ndicho kitabu!). Kwa
kawaida unaweza kuacha neno estas, yaani unaweza kujibu Jen gi!
tu.
99. MISEMO
Ujifunze misemo ifuatayo:
|
Kuna hali gani nje?
|
Kia estas la vetero ekstere?
|
|
|
|
|
Kumefunga mawingu.
|
Nubiĝis.
|
|
Kumekuwa
kweupe.
|
Klariĝis.
|
|
Inanyesha. Kunanyesha.
|
Pluvas.
|
|
Inaanguka
theluji.
|
Neĝas.
|
|
Kunakucha.
|
Tagiĝas.
|
|
Kumekucha. Kumepambazuka.
|
Tagiĝis.
|
|
Inaingia giza.
|
Noktiĝas.
|
Tulingoja hata imeingia giza.
|
Ni atendis
ĝis noktiĝo.
|
|
|
|
|
Basi, kwenye
misemo kuhusu hali ya hewa kwa Kiesperanto haitumiki kiwakilishi chochote cha
mtendaji. Pia katika msemo
huu:
Ŝajnas al mi, ke ...
|
Naona kwamba...
|
100. MAJINA YA HESHIMA
Kama Hamisi Saleh
ameoa Fatuma Kapinga na wao wamezaa Manase bin Hamisi Saleh, basi kwa
Kiesperanto:
Bibi Saleh
|
ni Sinjorino (S-ino ni kifupisho chake) Kapinga.
|
Mama Manase
|
ni Sinjorino Kapinga au Sinjorino Fatuma.
|
Bwana Hamisi
|
ni Sinjoro (S-ro) Saleh au Sinjoro Hamisi.
|
Bwana Manase
|
ni Sinjoro Saleh au Sinjoro Manase.
|
|
|
Bibi Nyanjala binti Hamisi Saleh
|
ni Sinjorino (S-ino) Saleh, au Fraŭlino
(f-ino) Saleh, au Sinjorino Njanĝala, au Fraŭlino
Njanĝala.
|
101. MAAMKIO
ANGALIA matumizi haya ya maneno Sinjoro, Sinjorino,
Fraŭlino:
Saluton, Sinjoro!
|
Jambo, bwana! Jambo, kaka!
|
Saluton, Sinjorino!
|
Jambo, mama! Jambo, bibi!
|
Saluton, Fraŭlino!
|
Jambo, bibi! Jambo, dada!
|
Lakini afadhali utumie neno saluton ukisalimu rafiki
tu, kama sivyo afadhali utumie maneno haya:
Bonan matenon!
|
Sabalkheri! Habari za asubuhi? (hutumika kuanzia asubuhi
mpaka adhuhuri)
|
Bonan tagon!
|
Sabalkheri! Habari za mchana? Habari za leo? (hutumika
wakati wa mchana baada ya adhuhuri)
|
Bonan vesperon!
|
Msalkheri! Habari za jioni? Habari za usiku? (hutumika jua
likianza kuchwa)
|
Bonan nokton!
|
Lala unono! Msalkheri! (hutumika jua likiisha kuchwa aghalabu
katika kuachana)
|
Maneno haya hutumika pia ukiachana. Katika kuachana na
rafiki hutumika pia Ĝis revido! (Kwa heri! Kwa herini!)
102. MISEMO
Parolu al la sinjoro.
|
Zungumza na bwana yule.
|
Mi konas tiun sinjorinon.
|
Namjua msichana (dada, binti) yule.
|
Ŝi estas ĉarma fraŭlino.
|
Yeye ni msichana (dada) mpendezi.
|
103 VIVUMISHI VINGINE
Kelkaj fraŭlinoj kantos.
|
Baadhi ya
wasichana wataimba.
|
Multaj floroj estas ruĝaj,
|
Maua mengi ni
mekundu,
|
aliaj estas bluaj.
|
mengine ni
buluu.
|
104. ZOEZI
Tafsiri ukitumia kamusi:
Mombaso, la 17-an de Decembro 1917-a
Kara amikino,
mi povas legi vian leteron; ĝi estas en la
internacia lingvo (lugha ya kimataifa) Esperanto. Ankaŭ mi havas
lernolibreton. Per la helpo de tiu libreto mi jam lernis sufiĉe por
skribi ĉi tiun leteron. La libro estas tre klara, kaj mi lernas rapide.
Esperanto estas tre simpla kaj interesa. Ankaŭ via frato devas aĉeti
libron kaj lerni la lingvon.
Hieraŭ mi ricevis belan ilustritan (-enye picha)
poŝt-karton de knabo, kiu loĝas en Nederlando (Uholanzi),
kaj mi povis legi ĝin facile per la helpo de vortareto. Morgaŭ mi
skribos leteron al japana knabo (mvulana mjapani). Mia fratino ofte
korespondas kun knabinoj en aliaj landoj. Ŝi nun havas multajn poŝtkartojn
kaj fremdajn poŝtmarkojn (stempu).
Kun koraj salutoj (Kwa salamu za moyoni),
Tumaini Mafuru
105. MAZOEZI:
Tafsiri ukitumia kamusi:
Londono, la 25-an de Julio 1982-a
Mia kara onklino,
mi dankas vin pro (kwa) la bela pupo, kiun vi
sendis al mi. Mi multe amas ĝin: ĝi havas bluajn okulojn kaj
ruĝajn vangojn, kaj ĝi povas fermi la okulojn.
Mi estas tre feliĉa ĉi tie. La floroj en la ĝardeno estas belaj.
Kelkaj pom-arboj (mtufaha
wa kizungu) estas en la ĝardeno, sed la frukto ne estas matura. Estas (Wapo)
kokoj kaj kokinoj sur la korto, kaj ŝafoj kaj bovinoj sur la granda kampo.
Ni ludas en la ĝardeno. Kiam (taz. vifungu vya 76 na
vya 87: Wakati
–po-, Ambapo) mi estas laca, mi sidas sur benko sub la arboj kaj legas. La
birdoj kantas sur la arboj, kaj belaj papilioj flugas en la ĝardeno. Mia
avo ofte sidas sur granda seĝo apud la fenestro, kaj legas gazeton aŭ
libron. Li havas multajn librojn. Sed mi devas fini mian leteron, ĉar mia
kara avino diras, ke (kwamba) mi devas nun iri al la lito. Bonan nokton!
Via amanta (akupendaye) nevino,
Ethel Brown