http://www.vessella.it KARIBU!
Jifunze lugha ya Kiesperanto

YALIYOMO

Utangulizi

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la kwanza

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la pili

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la tatu

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la nne

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la tano

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la sita

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la saba

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la nane

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la tisa

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18
Somo la kumi

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18

Kamusi

Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 18


Notice: Undefined variable: function_ret in /var/www/vhosts/vessella.it/httpdocs/fpdb/esp/yaliyomo.inc.php on line 43

4. SOMO LA NNE

24. KITENZI

Kitenzi kinaonyeshwa kwa kiambishi cha mwishoni -i kinachofanya kazi ile ile ya kiambishi awali cha Kiswahili ku-:

danci

kucheza dansi

legi

kusoma

dormi

kulala (usingizi)

ludi

kucheza

esti

kuwa

plori

kulia (machozi)

kanti

kuimba

ridi

kucheka

kuri

kupiga mbio, kuimbia

sidi

kukaa, kuketi

kuŝi

kulala (chini)

skribi

kuandika

labori

kufanya kazi

stari

kusimama

Lakini angalia kwamba unapotumia neno la kitenzi lenye kiambishi awali ku ili kuonyesha kitenzi kinapofanya kazi ya jina peke yake, kwa Kiesperanto hutumika neno lenye kiambishi cha mwishoni -o:

Kuimba kwa Juma ni kubaya.

La kanto de Ĝumo estas malbela.

25. KIAMBISHI TAMATI -AS

Kiambishi kinachoonyesha kwamba tendo latendeka wakatí huu wa sasa, au kwa kawaida. Nikisema La pano estas sur la tablo, ninafikiri wakati huu huu wa sasa. Angalia pia kwamba nikisema kwa Kiswahili "nimelala" ninafikiri wakati huu wa sasa sawasawa na "ninalala" au "nalala"; kwa hiyo:

Li dormas = Analala, Alala, Hulala, Amelala

Li staras = Anasimama, Asimama, Husimama, Amesimama

26. MTENDAJI

Mifano ya kifungu cha 25 yakuonyesha kwamba kwa Kiesperanto haitumiki kiwakilishi cha mtendaji kama a- (alala, analala, amelala = Li dormas) bali hutumika neno la li, yaani lazima kutaja kila mara jina lenyewe la mtendaji au badala yake maneno haya:

MI = mimi, ni-, n-, si­-

VI = wewe, u-, w-, hu-

LI = yeye, a-, yu-, n.k. (kwa wanaume tu)

SI = yeye, a-, yu-, n.k. (kwa wanawake tu)

ĜI = yeye, ki-, i-, n.k. (kwa vitu na wanyama)

NI = sisi, tu-, tw-, hatu-

VI = ninyi, m-, mw-, ham-, hamw-

ILI = wao, wa-, vi-, zi-, n.k.

27. ZOEZI

Tafsiri kwa Kiswahili:

Mi sidas kaj skribas. Li kuŝas kaj ripozas (kupumzika). Ni staras kaj legas. Ŝi estas en la ĉambro. Kie ĝi dormas? Mi sidas. La hundoj kuras. La birdoj flugas (-ruka). La kato kuŝas sur la lito. La knabo dormas en la lito.

28. ZOEZI

Kiu estas vi? Wewe ni nani?

Mi estas Aŝa. Mimi ni Asha.

Tafsiri kwa Kiswahili:

Kiu kantas? Ŝi kantas. - Kiu estas malbona knabo? Li. - Kiu parolas (-ongea, -zungumza)? Vi.

29. NENO NE

Neno hilo ndilo la kukanusha. Kwa Kiswahili habari ya kutotenda huonyeshwa kwa mabadiliko ya maneno ya matendo: ninasoma - sisomi; anafanya kazi - hafanyi kazi; kwa Kiesperanto lazima tutumie neno la kukanusha ne mara moja kabla ya jina la matendo (au jina lolote la kukanushia). Angalia katika sentensi zifuatazo jinsi neno la kukanusha linavyotumika:

Mwalimu hasimami.

Instruisto ne staras.

Walimu hawasimami.

Instruistoj ne staras.

Moyo ule haupigi.

La koro ne batas.

Mioyo ile haipigi.

La koroj ne batas.

Chakula hakitoshi.

Manĝaĵajo ne sufiĉas.

Vyakula havitoshi.

Manĝaĵajoj ne sufiĉas.

n.k.

k.t.p. (kaj tiel plu)

30. ZOEZI

Tafsiri kwa Kiswahili:

La pano ne sufiĉas. Ĝi ne estas freŝa. Ŝi ne estas bela, sed ŝi ne estas malbela. Ili ne ploras, ili ridas. Vi ne laboras, vi ludas. Mi ne staras sur la benko, ni sidas sur ĝi.

31. VlONGEZI

Kwa Kiswahili maongezo ya maana ya sentensi inawezekana kupatikana kwa kubadili mwisho wa kitenzi (hasa kwa jinsi ya kufanyia) au kwa kutumia maneno kama kwa, na, kwa ajili ya, kabla ya, baada ya, karibu na, juu ya, chini ya, n.k. maneno haya yaitwa kwa Kiesperanto "prepozicioj" na katika sarufi hii tutayaita "viongezi" kwa Kiswahili. Kiongezi ni namna moja ya viunganishi.

32. APUD = karibu na

Tafsiri kwa Kiswahili:

La teo estas apud la kafo. La hundo dorrnas apud la fenestro. Li sidas apud ŝi. La lito staras apud la muro.

33. SUB = chini ya

Tafsiri kwa Kiswahili:

Ili sidas sub la luno. La planko estas sub la plafono. La skatolo (mkebe) estas sub la tablo.

34. AL

Al huwa inaonyesha jinsi ya kufanyia tendo lenyewe lilivyo. Kwa kusema kweli mara nyingi vitenzi vya kufanyia haiwezekani kuvitafsiri kwa kutumia kiongezi al. Chungua sentensi zifuatazo:

Ninakutakia...

Mi deziras al vi...

Tunawasomea.

Ni legas al ili.

Unamzungumza nani?

Al kiu vi parolas?

Ninakwenda sokoni.

Mi iras al bazaro.

Ametuletea machungwa.

Li portis oranĝojn al ni.

LAKINI

Ametununulia machungwa.

Li aĉetis oranĝojn por ni.

Utuombee!

Preĝu por ni!

Msinilililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.

Ne ploru pro mi, sed ploru pro vi mem kaj pro viaj infanoj.

Kumtolea Mungu sadaka.

Oferi je Dio.

Ninakusalimia.

Mi salutas vin.

35. ZOEZI

Tafsiri kwa Kiswahili:

Ili kuras al ni. Ŝi kantas al li, sed li ne kantas al ŝi. La hundoj kuras al la knabo. La birdoj flugas al la arbo.

 

< Somo lililotangulia - Somo lifuatalo >
© Nino Vessella , 1996-.
Diritti riservati. Nessuna parte può essere riprodotta, in qualsiasi forma o mezzo, senza citare la fonte.
Ĉiuj rajtoj rezervitaj. Neniu parto povas esti reproduktita, en kiu ajn formo au per kiu ajn metodo, sen mencii ĉi tiun fonton.
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kunakili sehemu yoyote bila kuitaja asili yake hii.
All rights reserved. No part may be reproduced, in any form or by any means, without mention of this source.